UCHAWI

HAYA KWA WALE MSIO AMINI KAMA UCHAWI UPO JARIBU NA HAPA.
JINSI YA KUITA MZIMU NA KUUTUMA UNACHOKITAKA.
Nenda katika mti wa mwembe dodo unauchimba ukiwa uchi kisha unaufunga kamba na unauvuta kutoka kwa hiyo shimo mpaka mahali ulipovulia nguo kwa kutumia mguu.Wakati
unauvuta unasema kama anavyokuvuta wewe naomba ukanivutie mzimu wa makaburini wa mtu yeyote na ukamvute kwa nguvu zote na unaburuza mpaka ulipovulia nguo urefu wa mita tano kisha ufungue na uvae nguo zako kisha unaenda nyumbani,ukifika nyumbani ulaze nje.Kumbuka kazi hiyo unaifanya usiku kuanzia saa
mbili na kuendelea.Mzizi huo utauanika upondeponde kisha uusage ukishakauka..
Chukua mashahidi ya makaburi saba,saga changanya na huo mzizi wa mwembe.
Mzizi wa mbaazi ulio maliza mwaka.
Kivumbasi kilichoota kaburini changanya na udi za wormwood na sandalwood kisha unga huo utautumia kama ubani.Utachukua unga awa chaki nyeupe uchore sako ilioko hapo mbele kwa kutumia unga huo kwa chaki nyeupe au pemba nyeupe na utawasha mishumaa ya kijani mitano ,utaiweka kila kona ya sako na katikati ya hiyo sako utaweka mchanga wa kaburi wa huyo unayemuita au picha yake kisha utaanza kumuita Fulani Fulani Fulani njoo mimi Fulani nakuita nataka nikutume au unitimizie ninayotaka njoo kama rafiki mwema usinitishe basi ukifanya hivyo kwa muda atakuja na umwagize unachokitaka kiwe cha kheri au cha sharri.
Wakati huo unamuita utakuwa umeandaa fimbo ya mzizi wa muembe dodokwa ajali ya kumuondosha utakapomaliza mazungumzo naye maana usipofanya hivyo anaweza kukuganda hata ukienda sokoni unaena naye.Kumbuka kabla ya kumuita fanya zoezi ya kumuwaza na uonoe mawazo mengine kabisa.
ONYO Kama wewe ni mwoga usijaribu kufanya hii kazi maana huja kwa vitisho maaana huo unaoita ni mzimu.
Unapokuwa unamuita uwe umevaa kaniki nyeusi.

Na muda mzuli wa kufanya kazi hii ni usiku wa ijumaa kuamkia juma mosi usiku wa giza,. Anaweza kuja kama kivuli au anaweza kuja ana kwa ana na pia anaweza kuja moja kwa moja mkaonana akikuona sio muoga.
Mzimu huo unaweza kukuomba chakula mfano kama alikua anavuta ugoro au tumbaku au alikua anapenda chai au pombe nk. Hivyovitu unatakiwa uviandae uweke karibu na unapo fanyia kazi

Maoni

  1. Sijaelewa wormwood na sandalwood na maana ya sako kivumbasi nini nini na mashahidi ya makaburi ni nini

    JibuFuta
  2. Naomba pia kujua vitu unavyoweza kuutuma

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya kujua nyota yako kwakutumia tarehe yako ya kuzaliwa

TAFSILI ZA NDOTO MBALI MBALI

TAREHE YAKO YA KUZALIWA NA MAANA YAKE.